WAKURUGENZI WATAKIWA KUTOA TAARIFA KUHUSU MADAI YA WALIMU
WAKURUGENZI WATAKIWA KUTOA TAARIFA KUHUSU MADAI
YA WAKIMU
…………………………………………….
Wakurugenzi wa Jiji, Manispaa, Miji pamoja na
Halmashauri za Wilaya watakiwa kuandika barua kwa walimu ambao madai yao
yalikataliwa au kupunguzwa ili kuwapa taarifa sahihi kuhusu madai hayo.
Hayo yamesemwa na Kaimu Katibu Mkuu wa Ofisi
ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma Bw. HAB Mkwizu alipokuwa akiongea na
waandishi wa habari leo jijini dare s salaam kuhusu madai na madeni ya
watumishi wa umma.
Bw. Mkwizu amesema kuwa Serikali imekuwa
ikishughulikia madai na madeni ya watumishi wa umma kwa kuzingatia sheria,
kanuni na taratibu zinazotawala utumishi wa umma.
“Madai na madeni ya watumishi wa umma
yamegawanyika katika makundi mawili, madai yanayohusu mshahara ambayo hutokana
na mtumishi kuchelewa au kutokurekebishiwa mshahara pindi apandishwapo cheo
pamoja na madai yasiyohusu mshahara ambapo mwajiri huchelewa kulipa gharama za
likizo, masomo matibabu na uhamisho” alifafanua Bw. Mkwizu.
“Kwa upande wa walimu Serikali imekuwa
ikifanya kazi kwa kushirikiana na Chama cha Walimu Tanzania (CWT) ili kuweza
kufanikisha ulipaji wa madai ya walimu na hii haimaanishi kuwa madeni ya
watumishi wengine yamesahaulika” aliongeza Bw. Mkwizu.
Aidha, walimu wapatao 45,453 wanamadai ya
malimbikizo ya mshahara ya shilingi 32,104,487,430, hadi kufikia Septemba mwaka
huu Serikali imewalipa walimu 3,379 jumla ya shilingi 2,387,451,410 na walimu
wapoatao 1,667 wenye madai ya shilingi 1,733,641,362.7 watalipwa mwezi huu wa
octoba, alisema Kaimu Katibu Mkuu huyo.
Hata hivyo pamoja na jitihada zilizofanyika za
kuboresha Muundo wa Maendeleo ya Utumishi wa Walimu baadhi ya waajiri
hawajatekeleza kikamilifu muundo huo hivyo wametakiwa kutoa kipaumbele kwa
kuwapandisha madaraja walimu wapatao 41,700 waliogota katika muundo uliopita.
Comments
Post a Comment